10 May 2010
![]() |
| Timu ya chelsea jana iliibuka kidedea kwa kuigalgaza Wigan mabao 8-0 huku ikiwa imejiwekea mazingira mazuri ya ubigwa dhidi ya wapinzani wao wa ukaribu katika mbio za kuutwaa uchampioni wa ligi ya Uingereza msimu huu Man U.Wafungaji kwa vijana wa Stanford Bridge walikuwa ni Nicolas Anelka goli,Ashley Cole, na Solomon Kalou wote alifunga goli moja kila mmoja,wakati Frank Lampard akipachika magoli 2,huku Didie Drogba akipiga goli tatu na kuwa mfungaji bora wa ligi kwa kufikisha magori 29,akifuatiwa na Wayne Rooney Man U magoli 26. Mechi zingine zilizopigwa jana iliwakutanisha Man U dhidi ya Stoke city katika uwanja wa Old Trafford ambapo Man walishinda 4-0,Arsenal waliichapa Fulham 4-0 kataka uwanja wao wa Emirates,huku Liverpoor ikilazimishwa sale tasa na vibonde Hull city. |















