16 April 2010
![]() |
| Rapper 50 Cent ambaye sasa ni muigizaji ametangaza rasmi nia yake ya kufuta baadhi ya tattoo zake za mkononi. Tattoo hizo ambazo zimekuwa zikiuza kwenye picha za cover za album zake sasa zimeonekana kuanza kumkosesha mkwanja rapper huyo. Amesema ameshindwa kucheza muvi kibao kutokana na tattoo hizo kuonekana na amekuwa akitumia muda mwingi kuzificha kwa kupaka make up. 50 amesema ni bora azifute tattoo hizo ingawa ni gharama kubwa kufanya hivyo. |















