18 March 2010

Wanafunzi wa shule ya DIS wamechangia Shilingi milioni 1.5 katika kampeni zinazoendeshwa na mbunifu maarufu nchini Ally Rhemtulla pamoja na kampuni ya simu ya zain itwayo Fashion for Education,..
Kampeni hizi ni maalum kwa kuchangia mfuko wa elimu wa shule za sekondari za Kisarawe. Msaidizi mkuu wa shule hiyo Ms. Angelika Hub-bwana alisema wanayo furaha kubwa kuweza kuzisadia shule zingine ziweze kujitosheleza na vifaa vya kusomea. Pia muandaaji wa kampeni hiyo Ally Rhemtulla aliushukuru sana uongozi wa shule hiyo pamoja na wanafunzi wake.














