30 August 2010
![]() |
|
Ijumaa iliyopita jijini Nairobi Kenya, Raisi wa nchi hiyo Mwai Kibaki alizindua katiba mpya ya serikali ya Kenya . Sherehe hiyo ambayo ilihudhuriwa na umati mkubwa wa watu, ilingiwa na kasoro pale ilipobainika kuwa kiongozi na raisi wa Sudan bwana Omar al-Bashiri alikuwa ni mmoja wa wageni waalikwa katika sherehe hiyo. Rais Bashir anatuhumiwa na mahakama ya Kimataifa (ICC) kwa kukiuka haki za binaadamu katika serikali yake hasa upande wa Sudan ya Kusini wakati ikisemekana zaidi ya watu 300,000 wamepoteza maisha yao huko Darfur. Kenya inalaumiwa kwa kitendo chake cha kumualika kiongozi huyo , huku ikijua fika kwamba kama mwanachama wa mahakama hiyo ilitakiwa kumkamata kiongozi huyo ili akajibu mashitaka yanayomkabiri lakini ikashindwa kutekeleza wajibu huo. Bashir amekuwa akisakwa na mahakama hiyo toka mwaka 2009. Hata hivyo waziri wa mambo ya nje wa Kenya ametetea mwaliko wa Bashir kuwa haukuwa na madhara yoyote ambayo yangehatarisha usalama . |
|
|
|
SHOULD KENYA BE BANNED BY ICC ? Sudanese president faces charges of genocide and crimes against humanity in connection with violence in Darfur, where UN officials estimate 300,000 people have died. |
















